BUCADOS-Bukoba Catholic Diocese Orphans Scholarship ni shirika liloanzishwa na Jimbo Katoliki la Bukoba nchini Tanzania kwa lengo la kusaidia kusomesha watoto yatima na wenye uhitaji jimboni Bukoba,mkoani Kagera. BUCADOS inajishughulisha hasa katika kuchangisha fedha kutoka kwa wafadhili (Marafiki wa BUCADOS) kwa ajili ya kulipa karo na mahitaji mengine ya shule kwa watoto yatima kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.
Kauli Mbiu yetu Ili Wawe na Uzima ambayo ni msingi wa shughuli zote za BUCADOS inatokana na maneno ya Bwana Wetu Yesu Kristo: "Mimi nalikuja ili wawe na uzima" (Yohana 10:10). Tunatafsiri utume huu wa Kristu kuwa ndio utume wa Kanisa na kwa hakika ndio utume wa kila mbatizwa, kushiriki katika kazi ya wokovu; kujitoa kwa ajili ya maisha ya wengine. Maisha katika maana yake kamili yanajumuisha ustawi wa mtu kiroho (uzima wa milele) na kimwili (elimu, chakula na malazi). Hivyo basi, kumsomesha mtoto au mtu mwingine mwenye uhitaji, ni kuwaandalia msingi imara wa maisha; kuwapa uzima.
Wapendwa Familia ya Mungu,
Uhumuhimu wa elimu katika maisha ya mtu na hasa yatima ni mkubwa sana. Mtakatifu Matayo anatwambia: “Yesu aliwaonea huruma kwa kuwa walikuwa wamechoka na kudhoofika kama kondoo wasio na mchungaji” (Mt 9:36). Yatima wanapokosa fursa ya kusoma, wanatawanyika kama kondoo wasio na mchungaji na kuishia mitaani, wakiombaomba na kutumbukia katika uharifu, na kuwa wathirika wa madawa ya kulevya, kutumikishwa, unyanyasaji wa kijinsia na biashara ya binadamu. Jimbo Katoliki la Bukoba limekuwa kila mara mstari wa mbele katika kusaidia maskini wakiwemo yatima. Tunamshukuru Pd. Achilles Kiwanuka Macvhumilane kwa wazo la kuanzisha shirika la BUCADOS ili kusaidia kusomesha yatima. Nimetamani jambo hili siku nyingi kwa sababu mimi mwenyewe nilikuwa yatima, na hivyo nafahamu madhira wanayopitia yatima katika maisha yao. Kama methali isemavyo: “Usimpatie mtu samaki bali mfundishe kuvua,” tunatumaini kuwa kupitia BUCADOS, yatima watapata elimu na ujuzi wanaohitaji ili kujitengenezea maisha yao ya baadaye na kushiriki katika maendeleo ya jamii yao. Kwenu nyote na kwa wale wote watakaoifahamu BUCADOS kupitia kwenu, nawatakia Baraka za Mwenyezi Mungu na kuwaalika kutuunga mkono kwa kuchangia chochote kidogo ulichonacho ili kuisaidia BUCADOS katika malengo yake na kwa pamoja tuweze kushiriki katika utume wa Bwana wetu Yesu Kristu kama asemavyo: “Nimekuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele” (Yn 10:10); na kutimiza utume aliotuachia akisema “waacheni watoto waje kwangu” (Mt.19:14). Mungu na awabariki.
Coming Soon
Coming Soon
Padre Achilles Kiwanuka Machumilane mwanzilishi wa BUCADOS ni padre wa Jimbo Katoliki la Bukoba nchini Tanzania aliyezaliwa na kukulia Bukoba. Akiwa na umri wa miaka 8, Pd Achilles na ndugu zake walikuwa yatima kufuatia kifo cha baba yao, Mzee Dominic Rutakulemberwa aliyewaacha mikononi mwa mama yao Bertha Banagwa ambaye alikuwa mke wa nyumbani tu bila kipato chochote cha kiuchumi. Miaka iliyofuata ilikuwa ya shida kubwa kwa Pd Achilles na familia. Hapa chini, Pd Achilles anatushirikisha mapito aliyopitia akiwa yatima ambayo ndiyo sababu iliyomfanya aanzishe BUCADOS. Soma zaidiKusaidia kusomesha yatima maskini na watoto wenye uhitaji jimboni Bukoba ili kuwaandaa kushiriki katika kutatua changamoto za kiuchumi.
Tunakaribisha msaada wa kifedha kutoka kwa watu binafsi na mashirika, kupitia Bank Transfer, Credit Card na PayPal.
Unakaribishwa kujiunga na Marafiki wa BUCADOS ili usaidie kuchangia na kueneza lengo la BUCADOS ili kuwafikia wafadhili wengi zaidi.
Copyright © 2024 Bukoba Catholic Diocese - All Rights Reserved
Designed by Creative Mind