Lengo Letu

Kusaidia kusomesha watoto yatima na wenye uhitaji katika jimbo la Bukoba ili kuwatayarisha waweze kuchangia katika kutatua changamoto za kiuchumi zinazokabili familia zao na jamii yao na kushiriki katika utume wa Kanisa kwa ajili ya wokovu wa watu.

Malengo Mahususi

BUCADOS inalenga kuwawezesha watoto yatima na wahitaji jimboni Bukoba kupitia elimu kwa kuwalipia karo na mahitaji mengine ya kimasomo. Malengo mahususi ya shirika hili yatajumuisha yafuatayo:
  1. Kuomba na kuchangisha fedha kutoka kwa wafadhili binafsi na mashirika ili kusomesha watoto yatima na wahitaji jimboni Bukoba.
  2. Kuanzisha na kuendesha shughuli za kiuchumi ili kuongeza kwenye fedha zilizochangwa katika kusaidia elimu ya watoto yatima na wahitaji.
  3. Kutoa ushauri nasaha kwa yatima ili kuwawezesha kukabiliana na changamoto za kisaikolojia zinazotokana na kufiwa na wazazi.
  4. Kuzisaidia familia za watoto yatima wanaosaidiwa na BUCADOS kuanzisha shughuli za kiuchumi zitakazowasaidia kujitegemea na kuwasaidia watoto wengine ambao hawasaidiwi na BUCADOS.









Lengo la Shirika

Kusaidia kusomesha yatima maskini na watoto wenye uhitaji jimboni Bukoba ili kuwaandaa kushiriki katika kutatua changamoto za kiuchumi.

Soma zaidi


Saidia

Tunakaribisha msaada wa kifedha kutoka kwa watu binafsi na mashirika, kupitia Bank Transfer, Credit Card na PayPal.


Soma zaidi


Jiunge Nasi

Unakaribishwa kujiunga na Marafiki wa BUCADOS ili usaidie kuchangia na kueneza lengo la BUCADOS ili kuwafikia wafadhili wengi zaidi.

Jiunge


Copyright © 2024 Bukoba Catholic Diocese - All Rights Reserved

Designed by Creative Mind